(UFUNUO) MOYO WA JIWE
UFUNUO:
MOYO WA JIWE*
![]() |
| facebook :- (Ng'e Amazing Gospel) |
*EZEKIELI 36:26*
_“Nami nitawapa ninyi moyo mpya, nami nitatia roho mpya ndani yenu, nami nitatoa moyo wa jiwe uliomo ndani ya mwili wenu, nami nitawapa moyo wa nyama.”_
Swali je kwa mkristu katika Yesu tuna moyo wa jiwe au moyo wa nyama,
Jibu swali hili kwanza kwa hoja ya maandiko kisha weka notes zako pembeni sasa tuamze
*MOYO לב Lamed na Bet*
- *ל Lamed* fimbo ya mwalimu, kuinua, kunyanyua.
Inaonyesha moyo ni kitu kinachoinuliwa kutoka chini, kinachoongozwa juu kuelekea mlango wa uzima.
- *ב Bet* nyumba, mwili, makao.
Moyo ni kitu kilicho ndani ya nyumba ya mwili, kikiwa bustani ya ndani.
Hivyo moyo unanyuliwa kupitia mlango, kuongozwa katika mamlaka ya uzima.
*HISIA NA KUANGUKA*
Hisia = kitu kinachonyanyuka kutoka moyoni.
Zinaweza kupingana na mkono wa haki na kuinua moyo katika tamaa.
*Zayin* = katika kuona ndipo kuna upanga unao kata kutoka agano. Mwanzo Hawa aliona akatamani. Hile tamaa ndio kuinuka kwa moyo.
*TAMAA KWA KIEBRANIA*
*תַּאֲוָה ta’avah* = hamu kali, shauku.
Mizizi yake ni *אוה avah* = kutamani, kutaka. Ni kuvuta kuliko unganishwa na pumzi.
Pumzi ni moto unaowaka. Kitu unacho kivuta katika hisia au macho yako kikiunganishwa na pumzi kinakuwa moto unaowaka ndani ya mwili. Moto huu kuzimika ni kwa vitendo.
*MITHALI 10:24* _“Tamaa ya mwenye haki itatimizwa.”_
Hapa ta’avah = shauku njema, inayolingana na mapenzi ya Mungu.
*MITHALI 21:26* _“Mtu mvivu hutamani siku zote, lakini mwenye haki hutoa wala hakosi.”_
*ZABURI 78:29-30* Israeli walitamani nyama jangwani.
Ta’avah = tamaa ya mwili, bila uzibiti ni kifo.
Kwa hivyo: *Tamaa* inaweza kuwa baraka au laana kulingana na mwelekeo wake. Katika muktadha wa Ezekieli na Yesu, tamaa mbaya ni ishara ya moyo unaoinuka kwa kiburi, lakini tamaa njema ni shauku ya kutenda mapenzi ya Mungu.
Kukatwa kutoka katika uhusiano asili na Mungu.
*LUCIFER NA KUANGUKA*
*EZEKIELI 28:17* _“Moyo wako uliinuka kwa sababu ya uzuri wako; umeiharibu hekima yako kwa sababu ya mwangaza wako; nimekutupa chini”_
*ISAYA 14:13-14* _“Nawe ulisema moyoni mwako, Nitapanda mpaka mbinguni, Nitakiinua kiti changu juu kuliko nyota za Mungu... Nitapaa kupita vimo vya mawingu, Nitafanana na yeye Aliye juu.”_
Hii ndio ilikuwa tamaa ya Lucifer. Uzuli wake ndio ulimpa kiburi akatamani kuwa juu ya muumba wake.
Swali kuu watu huuliza: Kama Lucifer alikuwa malaika alipata wapi hisia za uasi?
Jibu: Lucifer aliumbwa na moyo wa uelewa. Na huo moyo kama tunavyo ona ni Lamed inayo inuka kutoka katika mwili. Huo ndio ufahamu. Lakini hisia hile hile ndio kifungo cha ufahamu.
Binadamu pia ameanguka kwa hisia hile hile ya kutamani kilicho juu.
Lucifer anapo anguka anakuwa shetani.
Tazama anapo mshauri Hawa kuwa _“mtakuwa kama Mungu”_. Alitambua tamaa ndio iliyomuangusha. Anatumia siraha ile kumuangusha mwanadamu.
Hivyo shetani ni mkono unao angusha kutoka katika mkono wa Mungu, kutoka katika Lamed ya mafundisho au kuinuliwa kutoka chini kuelekezwa katika mlango wa haki.
*KWA HIVYO:*
Moyo ni bustani ndani ya nyumba ya mwili, unanyuliwa na Lamed kuelekea mlango wa uzima. Lakini hisia zikinyanyuka katika tamaa, moyo huanguka kama Lucifer.
Baada ya Adamu kuanguka moyo wa mwanadamu unapoteza Lamed lakini unabaki na hisia ya kunyanyuliwa. Na hicho ndio chanzo cha ibada. Mwanadamu toka kale anamtafuta Mungu kwa sababu moyo wake ulijengwa kuinuka kutoka kifo lakini mkono wa mashitaka una mremea.
Hivyo kupitia Ibrahimu Mungu anatia nguvu katika moyo herufi *Hei* pumzi ambayo ndio jiwe nguvu ya Mungu.
*NENO “MPYA” KWA KIEBRANIA NI חָדָשׁ chadash.*
*ח Chet* uzio, kinga. *ד Dalet* mlango, kuingia. *ש Shin* moto, nguvu ya kubadilisha.
Mpya = Uzio katika mlango wa utakaso.
*KWA KIEBRANIA, NENO JIWE NI אֶבֶן even: Alef–Bet–Nun.*
Lakini ukianza na *ה Hei* kisha *Alef–Bet–Nun*, tunapata *הֶבֶן heben.*
*אֶבֶן Even*
Jiwe = nguvu ya Mungu iliyowekwa ndani ya nyumba ili kudumu.
*AYUBU 6:12* _“Je! Nguvu zangu ni nguvu za mawe?”_ Hapa Ayubu anaongelea kustahimili pigo, sio ugumu.
Even = jiwe kama msingi, uthabiti, uimara. Maana ipo katika nguvu na sio katika ugumu.
*EZEKIELI 36:26* Mungu asema: _“Nitatoa moyo wa jiwe na kuwapa moyo wa nyama.”_
Hii ni hukumu. Wana Israeli walikuwa na moyo wa jiwe. Nguvu ya Mungu. Lakini wakitumia nguvu hiyo kwa kiburi.
Hivyo Mungu anasema nitatoa tegemeo la nguvu zenu.
Kwa tafsiri ya kawaida, jiwe ni kitu kisicho na hisia. Lakini katika muktadha wa Ezekieli, si kwamba Israeli hawakuwa na hisia. Walipenda miungu mingine, vinyago na tamaa zao. Bali walitumia *nguvu ya Mungu* vibaya.
Jiwe = nguvu ya msingi ya nyumba ya Mungu. Israeli walikuwa juu ya makabila yote kwa sababu ya nguvu hii, lakini waligeuza moyo wao kwa kiburi na ibada za sanamu.
*MOYO WA JIWE VS. MOYO WA NYAMA*
*Moyo wa jiwe* = nguvu ya Mungu iliyotumika vibaya, kiburi, kinga ya kabila lakini bila utii.
*Moyo wa nyama בָּשָׂר basar* = *Bet* nyumba + *Shin* moto + *Reish* mamlaka/kichwa.
Nyumba inayowashwa iwakayo moto kwa mamlaka → moto wa utakaso.
Mfano Misri ni mfano wa watu wa mwili. Nyumba inayo ongozwa kwa moto wa mamlaka.
Mungu baada ya kuwapa wana Israeli uhuru wa kutosha lakini wakawa wanatangatanga katika imani za makabila.
Anasema nitatia moyo mpya.
Mpya: uzio mlango wa utakaso.
Kisha anasema nitatoa moyo wa jiwe, tegemeo la nguvu zenu, na kuweka moyo wa nyama: nyumba iwakayo moto kwa mamlaka.
Mstali unaendelea na _“nitakuwa Mungu wenu nanyi mtakuwa watu wangu.”_
Apa sio kauli ya kuchagua bali Mungu anatumia mamlaka kamili kuweka watu wake katika agano.
Nyumba hii inatakasa katika utii au inateketeza katika uasi.
Hivyo *moyo wa nyama ni hukumu ya utakaso*.
Tukishakombolewa kwa neema katika Kristo tuna moyo wa jiwe.
Moyo ulio thabiti, ulio imara, ulio pita katika tanuru ya moto.
Ungeniuliza swali hili siku chache nyuma hapa ningekwambia mimi nina moyo wa nyama.
Na hii ndio mtazamo wa wakristo wengi kuwa moyo wa jiwe ni ugumu wa kuto kuelewa. Lakini ishu iko kinyume. Kuomba moyo wa nyama ni kuwa upo katika mwili. Nasi katika Kristo tuna mamlaka juu ya mwili



Comments
Post a Comment